Jumamosi, 1 Oktoba 2016

MECHI YA WATANI WA JADI

Mechi ya watani wa jadi  kati ya Simba na Yanga  imemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao  1-1. Yanga  ilikuwa  timu  ya kwanza kujipatia bao lake la kuongoza dakika ya 26 ya mchezo kupitia mchezaji wake mahiri Hamis  Tambwe.Bao hilo  lilileta vurugu kwa mashabiki wa Simba hadi kupelekea kung'oa viti  na kuvitupa uwanjani,,,katika vurugu hizo ilipekea mchezaji nahodha wa Simba Jonas Mkude kupigwa kadi nyekundu. Simba iliendelea kucheza ikiwa pungufu hadi dakika ya 87 ya mchezo,mshambuliaji Kichuya wa Simba alivyosawazishia  timu yake  kwa goli safi la mpira wa kona ulioingia moja kwa moja wavuni na kufanya matokeo kuwa  1-1.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni